Tathmini ya biashara ya chapati - hamasisha

Saturday, September 30, 2017

Tathmini ya biashara ya chapati

Biashara ya kupika na kuuza chapati ni fursa kubwa kwa wanawake haswa Dar es salaam,  kutokana  na upatikanaji wake wa haraka kwaajili ya kufungua kinywa kimetokea kuwa kitafunwa kinachopendwa na watu wengi. Kwa tathmini za kawaida biashara hii imesomesha watoto na kusukuma maisha ya mwanamke wa kitanzania.
Ukitaka kufanya biashara ya chapati unatakiwa uwe na,
  • Unga wa ngano 
  • Mafuta
  • Chumvu
  • pan
  • Jiko

Nk: Unga wa ngano kilo moja unatoa chapati 15 - 18.

Mambo ya muhimu ya kuzingatia ukitaka kufungua biashara hii ya kuuza chapati

Usafi,

Biashara yoyote ya chakula inagusa afya ya binaadamu. Usafi binafsi na mazingira ni muhimu kwa mfanyabiara huyu . Muonekano wa mfanyabiara wa chakula ndio utakao wafuta wateja au kufukuza.

Mazingira,

Eneo lako la kufanya biashara linatakiwa liwe safi na la kupendeza machoni pa mteja, huwezi kuuzia chapati karibu na mtaro au karo  . Tambua wateja wako ni wakina Nani, waelewe wateja wako.

1 comment: