Folic acid ( vitamin B) , imetengenezwa Katika mchanganyiko wa virutubisho ndani ya vyakula asilia na matunda inayounda kidonge ambacho kinapatikana mahospitalini pamoja na maduka ya dawa , uzuri wake folic acid unaweza kupata ukila vyakula kama dagaa, maharagwe, mboga za majani, njegere, matunda, mayai ya kuchemsha na vinginevyo . Folic acid husaidia katika umbaji wa viungo vya mtoto akiwa tumboni
Matokeo ya ukosefu wa folic acid
- Mama kupungukiwa na damu
- Kutoka kwa mimba au kuzaa kabla ya wakati
- Mtoto Kuzaliwa na ulemavu
- Mtoto kupatwa na magonjwa kama kichwa kuwa kikubwa, mdomo wazi, mgongo wazi
Mama anaenyonyesha anashauriwa kupendelea vyakula vilivyo na folic acid pamoja na mama anaetafuta mimba.