wema wa akiba - hamasisha

Thursday, May 25, 2017

wema wa akiba

Wachache wenye tamaduni ya kuweka akiba wanaona matunda yake kwa maendeleo yao. Pesa ni kitu muhimu kwa kila mtu ila isikutawale wala shida zake zisikutawale. Akiba aiozi !. Kuweka akiba inahitaji uwe na subira au heshima na pesa yako.maisha ya mtanzania wa kawaida yampasa ajibane na kuweka akiba kwa kile kidogo alichopata. Ustaharabu sio kwa muonekano na kile kikutokacho mdomoni . Hata pesa inahitaji ustaharabu. Ni nini faida za kuweka akiba sasa ?

Maendeleo binafsi na uboreshaji wa maisha yako kifedha


Kwa maisha ya mtu wa kawaida akiba ni ngao ya maendeleo yake kwa maana apatapo pesa kuna matumizi binafsi na familia kwahiyo huyu mtanzania akikwatua na kuweka pembeni akiba yake kwa malengo fulani bila kupandisha kiwango kwa matumizi yake ataiona Pesa   . Huwezi kujenga kwa siku moja kupitia mshahara wa 200,000tsh. Bado hujatoa matumizi na dharura. 

Ulinzi.


Pindi unapopata dharura akiba inakuwa mkombozi mbadala wa kukopa . Matatizo hayana taarifa wala majira akiba itakuepusha wewe kutokukopa mikopo mikubwa kutatulia matatizo. Kuna njia mbadala ya kuweka akiba njia ya kudunduliiza, unaweza ukajiunga na insurance kwa ajiri na afya na mengineyo. 

uwekezaji


Kipaumbele cha Kwanza cha kuongeza kipato ni kupitia uwekezaji ila ntaanzaje kuweza kwenye Biashara bila mtaji?  Ukitaka kuwekeza tafakari na kuchanganua mpango wa Biashara kisha weka mlengo. Akiba huingia pale unahitaji kianzio. Hata kununua hisa inakuhitaji uwe na Pesa! Ntapataje Pesa , "akiba" 


No comments:

Post a Comment